Sunday, November 18, 2007

HARUSI YA BW. RICHARD MASUKE NA BI DINNA-Peace Of Mind TPDC Mikocheni tar 17 Nov,2007

"..kubyaala mawe,kubyaala cha widza..."
ilikuwa ni uhondo kutoka kwa DJ TEN akiwakamata wasukuma kwa kina walipokuwa wakiwa na furaha ya kupata binti mrembo mwenye asili ya kijita,aliyezamia mitaa ya Bariadi siku tele na kuwa na ladha ya kisukuma pia-Dinna..mweupe na ambaye kwa mila za kisukuma basi hiyo mahali yake ukiwa namfuko mwepesi hugusi. Ila kijana Richard akajipindua na kumtia kibindoni kwa furaha za ziada.
"...ndolelaaaaa...ndolela babaaaa...!" wasukuma wa kijita hao wakazunguka nao wakijifariji baada ya binti yao kuungana na familia ya kina Masuke.Wakicheza kwa furaha na kuongozwa na Ephraim Mafuru(Marketing manager wa Vodacom Tanzania),paliwa hapatoshi!!
Mtaalamu wa burudani McNdimbo,kama kawaida akiwapa wakati mgumu weasukuma wala kuketi katika viti vyao kila baada ya muda! kwa kweli ilikuwa burudani kwelikweli.
Shughuli hiyo ilisheheni wadau wa kutosha akiwamo Waziri wa mifugo,Mh.Diallo

SEND OFF PARTY YA BI.ABELA KAJUMULO LANDMARK HOTEL TAR 8,NOV,2007

Ilikuwa ni nderemo na furaha kwa wahaya wale na kuwa na uhakika na kupata mume tena wa kinyumbani! ilikuwa ni '...dereva babili...dereva babiliii eee...!' kili baada ya muda. wazazi wakiwa na furaha kweli na hasa Mama wa bibi arusi mtarajiwa a.k.a mama Tina,ambaye pia ni mama yake na mwigizaji maarufu wa filamu hapa nchini-Kanumba(ambaye alikuapo pia).
Shughuli ilianza na taratibu za mila na desturi za kihaya,wakwe wakaingia na mizigo ya kutosha;kabiya(beer),kasoda,bila kusahau kabhitoki(ndizi) na kakinywaji ka nyumbani. Ilikuwa ni burudani sana kuona wahaya hao,pamoja na usomi wao uliobobea,wakizama katika mila na desturi zao.
Baada ya majadiliano marefu ya hapa na pale kati ya mshenga na wazazi wa binti mtarajiwa waliruhusiwa kumleta bwana mtarajiwa ndani na kisha bi mtarajiwa akaingia kwa mbwembwe na shughuli ikaenda murua chini ya mikono salama ya mtaalam wa kuburrudissha hapa Africa ya mashariki na kati-McNdimbo 'mwana wa mshikemshike'
Pamoja nae alikuwapo Dr. Zero 'mzee wa dozi nene' kwa maharusi na show yake kali yenye vionjo vyote vya burudani;bongo flava,gospel,zilipendwa hadi segere! kudadadeki!!
ilikuwa ni uhondo toshaaa!