Sunday, April 8, 2007

SEND OFF-BEACHCOMBER

Pembezoni kabisa mwa jiji la Dar es salaam,katika ufukwe wa bahari ya Hindi,upepo mwanana ukivuma na kuruhusu wageni wapatao 200 kjisikia peponi kwani walikuwa wamezunguka bwawa la kuogelea la Hotel nzuri ya BeachComber huku kwa shauku kubwa wakimsubiri mrembo Bi Violet Rutashobya aingie na wapate fursa ya kumuaga.
Kazi nzuri ya upambaji kutoka Dotinata Decoration na burudani tosha ya muzik kutoka Vuje Disco Sound vilitosha kumfanya Mwana wa Mshikemshike aongee kwa kujiamini kuwainua wageni hao ili kumpokea Mtarajiwa huyo aliyepambwa na kupambika pale Sinza Mori Mary Saloon....
Hoihoi na nderemo hazikupotea baada ya hapo kwani burudani ndo ilikuwa jadi ya hapo!!

No comments: